7Sheria ya Bwana ni kamilifu, Huiburudisha nafsi. Ushuhuda wa Bwana ni amini, Humtia mjinga hekima.
8 Maagizo ya Bwana ni ya adili, Huufurahisha moyo. Amri ya Bwana ni safi, Huyatia macho nuru.
9 Kicho cha Bwana ni kitakatifu, Kinadumu milele. Hukumu za Bwana ni kweli, Zina haki kabisa.
10 Ni za kutamanika kuliko dhahabu, Kuliko wingi wa dhahabu safi. Nazo ni tamu kuliko asali, Kuliko sega la asali.
11 Tena mtumishi wako huonywa kwazo, Katika kuzishika kuna thawabu nyingi.
12 Ni nani awezaye kuyatambua makosa yake? Unitakase na mambo ya siri.
13 Umzuie mtumishi wako
asitende mambo ya kiburi, Yasinitawale mimi. Ndipo nitakapokuwa kamili,
Nami nitakuwa safi, sina kosa lililo kubwa.
14 Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu. Zab 19:7-14
lucinadeus
Monday, September 28, 2015
Monday, February 16, 2015
NIENDAVYO KWARESMA HII(nataka kuwa chumvi ya ulimwengu)
Habari wapendwa!
Jumatano tar 18/02/2015 ni siku tunayoanza mafungo katika Kwaresma.
Kila mwaka huwa tunafanya hivi,mwaka huu naona Mungu anasema nami kwa namna ya tofauti kwa habari ya malengo ya mafungo ya mwaka huu.
Nimejikuta natamani sana mwaka huu mafungo yangu yalenge hasa katika eneo la utumishi.Natamani Mungu anitengeneze na aseme nami kwa kina kuhusu utumishi na huduma aliyoniitia.Ninategemea kufanya yafuatayo kama sehemu ya mafungo yangu:
1.Kupata muda wa kutosha kuomba kwa kina sana.
2.Kusoma kwa bidii na kwa kina Neno la Mungu
3.Kuchochea karama yangu kwa maana ya kufanya kile kinochohusiana na karama yangu ili nipate kujifunza zaidi.
Ninakualika na wewe mwenzangu,eneo ambalo unaona Mungu anasema nawe likae sawa na bado unaona hujaweza kulitendea haki,fanya kitu kwaresma hii.
Ni maombi yangu kwa Mungu kwamba Kipindi hiki kisipite bure bali tuvuke kutoka eneo moja kwenda eneo lingine kwa utukufu wa Jina lake.Vile viwango ambavyo tumekuwa tunatamani kuvifikia tumsihi Mungu atufikishe hapo kwaresma hii.
Ninamwomba Mungu kabla ya kuanza kwa mafungo hayo niweze kujiaandaa kikamilifu na anipe Neema ya pekee itakayoniwezesha kufanya mafungo hayo kwa ukamilifu na kwa namna inakayompa yeye Mungu utukufu,AMEN.
**********nataka kuwa chumvi*********nataka kuwa chumvi *******
Monday, January 26, 2015
MAPENZI YA MUNGU
MAPENZI YA MUNGU- KUYAJUA NA KUYATENDA
KUYAJUA MAPENZI YAKE
KUYATENDA MAPENZI YAKE
KUYAJUA MAPENZI YAKE
1 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu
iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye
maana.
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu. Rum 12:1-2
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu. Rum 12:1-2
Msiipende dunia, wala mambo
yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.
Maana kila kilichomo duniani,
yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na
Baba, bali vyatokana na dunia.
Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele. 1 Yoh 2:15-17
Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele. 1 Yoh 2:15-17
Friday, December 19, 2014
TUNAWEZAJE KUOKOLEWA NA UHARIBIFU ULIOKO DUNIANI
Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili
kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu
uliomo duniani kwa sababu ya tamaa. 2 Pet 1:4
1.Tumekirimiwa ahadi kubwa mno za thamani
2.tupate tabia ya Uungu
tabia hiyo itatuwezesha kuokolewa na uharibifu huo
tabia hiyo itatuwezesha kuokolewa na uharibifu huo
Monday, December 1, 2014
LETA USHAWISHI KATIKA UFALME
Kulikuwa na semina jmosi tar 29/11/2014 inayohusu "kuendesha biashara inayoleta ushawishi katika ufalme wa Mungu".Nimejifunza mengi sana katika semina hiyo.
1.Ni muhimu sana kuwa na mtazamo sahihi(kuhusu unalotaka kufanya) tunapotaka kufanya bishara au kitu kingine.Katika biashara mimi kama Mkristo ninapaswa kuingia katika biashara nikiwa ni mtazamo unaolenga kwanza kuhusu ufalme wa Mungu mfano: sipaswi kuingia katika biashara kutafuta faida tu,kwanza nilenge kutumia bishara yangu kuhudumia jamii kwa namna mbalimbali mfano kwa kuboresha maisha ya watu,kutatua matatizo ya jamii husika na pia kuufanya ufalme wa Mungu uje katika mahali nilipo.Tutakapokuwa na mtazamo huo hata mtaji,wateja havitakuwa kazi kwetu,Mungu mwenyewe atashughulika na hayo maana ndivyo alivyosema katika Neno lake "Tafuteni kwanza ufalme wa Mungu,na haki yake na mengine yote mtazidishiwa".
Tunapaswa kufahamu kuwa sisi sio wamiliki wakuu wa biashara zetu.Kwa kuwa sisi ni mali ya Mungu,mmiliki mkuu wa biashara zetu ni Mungu,Tumkabidhi Yeye ili azitumie kwa utukufu wa Jina lake.
Mungu ametupa vipawa,ujuzi mbalimbali.Tunapaswa kuvitumia tukijua si mali yetu bali tumepewa dhamana na tutaulizwa tulivitumiaje kama mifano wa wale waliopewa talanta kwenye Biblia.
2. Kila Mtu ana vitu kwa ajili ya kizazi chake.Tumezaliwa navyo,kwa hiyo tusijidharau,tujitambue na kuwa na ujasiri wa kuanza kuvitumia kwa ajili ya utukufu wa Mungu.Tumezaliwa na suluhisho la matatizo mbalimbali.Tusilalamikie matatizo bali tutumie hayo kama changamoto ya kutusaidia kujua na kukuza vipaji vyetu.Je kwenye jamii inayokuzunguka unaona kuna mapungufu gani?unadhani unaweza kufanya nini kusaidia katika hayo?kumbuka wewe Mkristo ni nuru,wewe ni Chumvi unapaswa kuangaza.Jitambue,mshirikishe Mungu katika maisha yako umruhusu atawale kweli na kwa pamoja naye utaweza kutambua ulivyonavyo na kuleta ushawishi katika ulimwengu unaokuzunguka.
"Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake" Yoh 4:34
Mungu Mwema atubariki sote tunapoendelea kuyatafuta mapenzi yake katika yote .AMEN.
1.Ni muhimu sana kuwa na mtazamo sahihi(kuhusu unalotaka kufanya) tunapotaka kufanya bishara au kitu kingine.Katika biashara mimi kama Mkristo ninapaswa kuingia katika biashara nikiwa ni mtazamo unaolenga kwanza kuhusu ufalme wa Mungu mfano: sipaswi kuingia katika biashara kutafuta faida tu,kwanza nilenge kutumia bishara yangu kuhudumia jamii kwa namna mbalimbali mfano kwa kuboresha maisha ya watu,kutatua matatizo ya jamii husika na pia kuufanya ufalme wa Mungu uje katika mahali nilipo.Tutakapokuwa na mtazamo huo hata mtaji,wateja havitakuwa kazi kwetu,Mungu mwenyewe atashughulika na hayo maana ndivyo alivyosema katika Neno lake "Tafuteni kwanza ufalme wa Mungu,na haki yake na mengine yote mtazidishiwa".
Tunapaswa kufahamu kuwa sisi sio wamiliki wakuu wa biashara zetu.Kwa kuwa sisi ni mali ya Mungu,mmiliki mkuu wa biashara zetu ni Mungu,Tumkabidhi Yeye ili azitumie kwa utukufu wa Jina lake.
Mungu ametupa vipawa,ujuzi mbalimbali.Tunapaswa kuvitumia tukijua si mali yetu bali tumepewa dhamana na tutaulizwa tulivitumiaje kama mifano wa wale waliopewa talanta kwenye Biblia.
2. Kila Mtu ana vitu kwa ajili ya kizazi chake.Tumezaliwa navyo,kwa hiyo tusijidharau,tujitambue na kuwa na ujasiri wa kuanza kuvitumia kwa ajili ya utukufu wa Mungu.Tumezaliwa na suluhisho la matatizo mbalimbali.Tusilalamikie matatizo bali tutumie hayo kama changamoto ya kutusaidia kujua na kukuza vipaji vyetu.Je kwenye jamii inayokuzunguka unaona kuna mapungufu gani?unadhani unaweza kufanya nini kusaidia katika hayo?kumbuka wewe Mkristo ni nuru,wewe ni Chumvi unapaswa kuangaza.Jitambue,mshirikishe Mungu katika maisha yako umruhusu atawale kweli na kwa pamoja naye utaweza kutambua ulivyonavyo na kuleta ushawishi katika ulimwengu unaokuzunguka.
"Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake" Yoh 4:34
Mungu Mwema atubariki sote tunapoendelea kuyatafuta mapenzi yake katika yote .AMEN.
Thursday, September 18, 2014
Neno la leo
Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza. Bali kila anisikilizaye atakaa salama, Naye atatulia bila kuogopa mabaya
Mith 1:32-33
For the straying of the naive kills them,
Mith 1:32-33
For the straying of the naive kills them,
the smugness of fools destroys them.
But whoever obeys me dwells in security,
Thursday, July 19, 2012
UJUMBE J2 YA 14 MWAKA B
Mk 6:1-6
1.Tusimwangalie aletaye ujumbe pekee bali tupokee zaidi ujumbe utokao kwa Mungu
2.Tuangalie mambo kwa mitazamo ya kiroho si kimwili tu mfano tusidhani tumemfahamu Yesu tukashindwa kuona zaidi katika Roho
1.Tusimwangalie aletaye ujumbe pekee bali tupokee zaidi ujumbe utokao kwa Mungu
2.Tuangalie mambo kwa mitazamo ya kiroho si kimwili tu mfano tusidhani tumemfahamu Yesu tukashindwa kuona zaidi katika Roho
Subscribe to:
Posts (Atom)