Ikiwa jana ilikuwa ni sikukuu ya Ekaristi Takatifu,ningependa kuwashirikisha yaliyofundishwa nilipohudhuria ibada ya misa kigango cha Kiseke Parokia ya Ilemela.
Ujumbe wa jumapili sikukuu ya Ekaristi Takatifu.
Tunapompokea Yesu wa Ekaristi tunapaswa kufanana nae.
Swali la kujiuliza: kwa nini tunampokea Yesu mara kwa mara lakini hatubadiliki?bado tunapenda dhambi?tunafanya mambo yetu wenyewe badala ya kufanya yale anayotaka Mungu kama Yesu alivyokuwa anafanya?
Jibu:
1.Hatuna Imani ya Kutosha kwa Yesu
2.Hatujaamini uwepo wa Yesu katika Ekaristi Takatifu
Yatupasayo
Inatupasa tumwombe Mungu atuongezee imani kwake na kwa Yesu Kristo mwanae.
Mara
tutakapokuwa na Imani ya Kutosha (kubwa na thabiti) kwa Yesu na kuamini
uwepo wake katika Ekaristi Takatifu,tutamwabudu inavyopasa na kumpokea
kwa heshima na Uchaji mkubwa.
Yesu atakapokuwa ameingia katika
maisha yetu atayabadilisha yafanane naye na hivyo hatutakuwa tena sisi
tunaishi bali Kristo ndani yetu ndiye atakuwa akiishi katika maisha
yetu.
Wito
Ekaristi Takatifu inatupatia neema nyingi sana
tunazozihitaji katika maisha yetu.Neema ni msaada wa Mungu utuwezeshao
kutenda mema.Tumkaribishe basi Yesu wa Ekaristi mioyoni mwetu kwa
kupokea Ekaristi Takatifu katika hali ya usafi mara kwa mara ili
atujaze neema nyingi zitakazotusaidia kumpendeza Mungu katika maisha
yetu.
Baada ya kuwa tumemkaribisha Yesu katika mioyo yetu nakumruhusu atawale
maisha yetu,tunapaswa kumshuhudia na kumtangaza kwa watu wote.
Monday, June 11, 2012
Friday, June 8, 2012
JUNE PRAYER POINTS
Baadhi ya mambo ya kuombea mwezi huu
VIJANA
-Vijana tupate maono kutoka kwa Mungu kupitia Roho wake Mtakatifu (Mdo 2:14-18 )
-Maono yote Mungu aliyokwishatupa yakapate kutimia kwa wakati wake,Mungu afanye njia sawa sawa na Zab 33:10-11 (yataje hapa maono hayo)
-Nguvu ya Ujana itumike kumtukuza Mungu (1 Yoh 2:13-14)
KANISA
-Roho ya Hekima na Ufunuo katika kumjua Mungu (Ephe 1:17)
-Kumpenda Mungu na kumheshimu Mungu kweli kweli
-Kanisa tufahamu mamlaka na nguvu alizotupa Kristo na kutenda kazi yake kwa ujasiri (Efe 1:18-23)
-Watendakazi katika shamba la Bwana waongezeke: Mungu aachilie karama na fadhila zake kwa wingi zaidi na zaidi
TAIFA
Roho ya Hekima kwa viongozi
Moyo wa upendo viongozi
Umoja,upendo na amani kwa watu wote
ISRAEL
-Favour na Kibali cha Mungu viendelee kuwa pamoja nao
-Zab 33:10-11
WATU WOTE
-Paji la Imani kwa Yesu Kristo kwa watu wote
-Tufahamu ukweli na ukweli utuweke huru kweli kweli Yoh 8:32
-Neema ya wokovu
-Maono yote Mungu aliyokwishatupa yakapate kutimia kwa wakati wake,Mungu afanye njia sawa sawa na Zab 33:10-11 (yataje hapa maono hayo)
VIJANA
-Vijana tupate maono kutoka kwa Mungu kupitia Roho wake Mtakatifu (Mdo 2:14-18 )
-Maono yote Mungu aliyokwishatupa yakapate kutimia kwa wakati wake,Mungu afanye njia sawa sawa na Zab 33:10-11 (yataje hapa maono hayo)
-Nguvu ya Ujana itumike kumtukuza Mungu (1 Yoh 2:13-14)
KANISA
-Roho ya Hekima na Ufunuo katika kumjua Mungu (Ephe 1:17)
-Kumpenda Mungu na kumheshimu Mungu kweli kweli
-Kanisa tufahamu mamlaka na nguvu alizotupa Kristo na kutenda kazi yake kwa ujasiri (Efe 1:18-23)
-Watendakazi katika shamba la Bwana waongezeke: Mungu aachilie karama na fadhila zake kwa wingi zaidi na zaidi
TAIFA
Roho ya Hekima kwa viongozi
Moyo wa upendo viongozi
Umoja,upendo na amani kwa watu wote
ISRAEL
-Favour na Kibali cha Mungu viendelee kuwa pamoja nao
-Zab 33:10-11
WATU WOTE
-Paji la Imani kwa Yesu Kristo kwa watu wote
-Tufahamu ukweli na ukweli utuweke huru kweli kweli Yoh 8:32
-Neema ya wokovu
-Maono yote Mungu aliyokwishatupa yakapate kutimia kwa wakati wake,Mungu afanye njia sawa sawa na Zab 33:10-11 (yataje hapa maono hayo)
MKUTANO WA SALA NYAKAHOJA
Alhamisi hii masomo yalikuwa
Zaburi (Psalms) 103:1-22
Kutoka (Exodus) 23:27
Yeremiah Jer 30:16
Mungu ametukumbusha upendo wake usivyo na mipaka katika zab 103
Pia ametukumbusha kumwomba daima ulinzi kupitia Neno lake. na si ulinzi tu bali kila tuombayo tuombe sawa sawa na Neno lake linavyotuahidi.
Zaburi (Psalms) 103:1-22
Kutoka (Exodus) 23:27
Yeremiah Jer 30:16
Mungu ametukumbusha upendo wake usivyo na mipaka katika zab 103
Pia ametukumbusha kumwomba daima ulinzi kupitia Neno lake. na si ulinzi tu bali kila tuombayo tuombe sawa sawa na Neno lake linavyotuahidi.
Subscribe to:
Comments (Atom)